MAISHA YANAPOANZIA
Kuna tofauti kubwa kati ya yale tunayofikiri na yale mambo tunayoyajua rohoni mwetu. Kuna ulimwengu pana wa tofauti. Mazingila yetu ya mafikiri na uzoefu vya mda unaopita kwa nyakati zetu siyo ukamilifu. Dunia iliumbwa kama shamba linalokua, Linalo mwanzo, maisha na wakati wa mavuno. Wakati wa mavuno sio mwisho kabisa lakini ni mwanzo wa kujilikana kwa ukweli wa kila kitu.
Roho wetu ni nini? Ni "mahali pa kuishi kwa Baba" ambaye hawezi kuishi pamoja na kitu chochote. Roho wetu anaweza kusikia au kuhisi kitu fulani wakati ambapo fikirio zetu haziwezi kabisa. Busara za mafikirio ziko na mpaka lakini roho haina. Ndani yetu kuna pande takatifu ambalo linataka wakati wowote kujua ukweli na ni lenye nguvu kushinda uelekevu wetu jinsi ambavyo mafikiri yetu hayawezi gundua hata kidogo.
Roho wetu ni kiini cha wale tulio, katika mwili utakaokufa, Lakini mwili sio mpaka wake. Tumeumbwa. Hatukujiumba pekee zetu. Watu wengi wanajua ukweli huu hata ingawa iwe kwa kiwango kidogo. Tumeumbwa jinsi inayohofiwa na inayoshangaza. Nani ametupatia maisha? Nani alifanya siku za leo tuwe tukiishi? Nani aliye mwanzo wa ulembo wa kushangaza wa dunia hii?
Nani alimpatia kila mtu upekee wake? Ni Chenye uhai. Ni MTU. Mtu ambaye anaweza kuguswa au kusikilizwa na roho wetu na ndiye ambamo roho wetu anatokea. Ndiye anataka kutoa maisha ya kutosha, yanayojaa furaha, uzuri na upendo. Yeye ni maisha mwenyewe na anatoa maisha wakati wowote.
Kama vile tunavyotoa maisha kwa watoto wetu wakati wakizaliwa, na yeye ametupatia maisha sisi. Huyo mwenye uhai alikuwa anatuhitaji na alikuwa akitaka tukue, tutazame ulembo wa nyota angani, tuyafurahie maisha lakini juu ya hayo yote alikuwa akitaka tuje tupendwe na tena tupende.
Na hata katika upendo huo, tunapokua tukielekea mavuno, alikuwa anahitaji tumjue zaidi. Kumfahamu yeye ni kujua upendo jinsi ulivyo. Anataka tushike mkono wake tuwe tukitembea sambamba naye, tuongee naye naye ataongea nasi. Anahitaji tumfahamu kikamilifu kama vile yeye anatujua vizuli kabisa.
Sababu ya maisha na lengo la kuwepo ilikuwa tuje tujue ukweli na tumjali muumbaji wetu aliyetupatia uhuru wa kuchagua. Na sisi wakati tukingali hapa duniani, tunaweza tukachagua kuyajua yale tunayoyafikiri tu au tunaweza tukachagua kujua mengi zaidi. siku moja tutajua vilivyo yale mambo ambayo hatuwezi gundua vizuri tukingali hapa dunia na pia tutaijua vizuri dunia mpya, lakini tunaweza kuchagua kuyajua sasa hivi yale ambayo Baba wa mbinguni ataonyesha miwili yetu yakiroho.
Uhuru wetu wa kuchagua ulikuja kwa bei ghali kwa yule aliyetuumba. Jinsi tunavyochagua itaonekana au ikijaa upendo au ikijaa kujipendelea. Kujipendelea inatufanya kujivuna juu ya yote na kufanya hayo vinatutenganisha na maisha kama vile mashariki yanatengana kabisa na magharibu. Kuchagua kama hivyo inatuletea balaa na tunaona matokeo mabaya katika mazingila yetu.
Muumbaji wetu alikuwa hajitegemei kuona maisha mabaya, ambayo tulijijengea sisi kupitia katika matendo yetu au jinsi tunavyochagua vibaya. Ametuona tumezimia, tumetengana na soko letu. Kwa hivyo akaja kati yetu ili atuonyeshe tena soko letu, ili tukumbuke upendo rohoni mwetu. Ili aonyeshe upendo wa juu usio na uchafu wowote ambao aliuonyesha akiwa msalabani, upendo huo ulionyeshwa na Yesu mwenyewe. Mambo hayo yalitokea baada ya mda mrefu kutoka wakati wa uumbaji. Kila wakati Mungu alikuwa akifanya kila liwezekanalo ili turudie kwa ahadi zetu isipokuwa tu dunia hii wala miwili itakayokufa. Lengo lenyewe Mungu alilotuumbia ni tuje tukisikie huru toka minyololo ya hofu, matatizo, na maladhi.
Baba ameniambia "Mbinguni hakuna hosipitali au vituo vya maziko wala nyumba za wafungwa." Giza litakuwa limekwisha kwani tutakuwa ndani ya mwangaza. Tutakuwa tukisikirizana visivyodhihirika. Vimeandikwa msalabani. Mkifikiria juu ya Baba mfikirie juu ya yule aliyetuumba ili tuwe na matumaini ya furaha ya kujijua na kumjua yeye pia. Njoo kwake na shika mkono wake. Ongea na ye, naye ataongea nawe. Kwa ukweli hapo ndipo maisha yanapoanzia.